UFUGAJI WA NGURUWE UNALIPA: Huu Ndio Muda Sahihi wa Kuanza! 🐖💰

0


Katika harakati zetu Rubaba Media kuelimisha na kushauri wakulima na wafugaji kote nchini, tukishitikiana na Koudijs safari yetu ya hivi karibuni ilitufikisha mkoani Mara — hasa maeneo ya TarimeNyamongo, na vitongoji vyake. Tulikutana na wafugaji wapya na waliopo tayari waliodhamiria kwa dhati kuhakikisha ufugaji wa nguruwe unabadilisha maisha yao.

Lakini pia tuliona jambo moja la msingi: Ufugaji wa nguruwe bado haujachukuliwa kwa uzito unaostahili na watu wengi, ilhali ni moja ya sekta zinazolipa sana ukizingatia mahitaji ya soko la nyama na mbegu bora zinazoongezeka kila siku.


🐷 Mfano Hai wa Mr & Mrs George – Waanzilishi Wenye Maono


Wakiwa wakazi wa Tarime, Mr & Mrs George ni mfano bora wa familia mpya iliyodhamiria kuingia kwenye ufugaji wa nguruwe kwa maandalizi ya kisasa. Wameanza kwa kuchagua mbegu bora, kujenga banda la kisasa lenye uingizaji hewa mzuri na mazingira safi, na zaidi wamechagua kupata elimu ya kina kutoka kwa wataalam ili kuepuka makosa ambayo yamekuwa kikwazo kwa wafugaji wengi.


Wanaamini kuwa, kwa mipango sahihi, ufugaji wa nguruwe si tu chanzo cha kipato cha uhakika, bali pia njia ya kujenga biashara endelevu kwa familia.


🐖 Mr. Julias – Kutoka Nguruwe Wachache Hadi Mzalishaji wa Mbegu Bora


Mwaka 2021, Mr. Julias alikuwa na ndoto tu — alianza na nguruwe wachache katika kijiji chake Tarime. Leo hii, ni mmoja wa wazalishaji wakubwa wa mbegu bora za nguruwe katika kanda ya ziwa. Anauza majike na madume yenye afya njema, huku akiwa ni sehemu ya wafugaji wanaosaidia kuendeleza vizazi bora vya nguruwe Tanzania.


Aliamua kuwekeza kwenye elimu, lishe bora, na mbinu bora za usafi na uendeshaji wa banda. Matokeo yake? Anaingiza faida mara dufu, na ameongeza idadi ya wateja kila mwezi.


💡 Kwa Nini Uanze Ufugaji wa Nguruwe Leo?

  • ✅ Soko la nyama ya nguruwe linazidi kuongezeka nchini na nje ya nchi.

  • ✅ Faida ni kubwa ukilinganisha na gharama za kuanzia.

  • ✅ Nguruwe hukua haraka, na wana uwezo wa kuzaa mara kwa mara hadi watoto 12 au zaidi.

  • ✅ Hakuhitaji eneo kubwa sana kuanzisha.

  • ✅ Uzalishaji wa mbegu bora ni biashara inayolipa zaidi kadri mahitaji yanavyoongezeka.

🔍 Unahitaji Elimu, Ushauri au Mafunzo?


Katika kazi yetu ya kuzunguka Tanzania nzima, lengo letu ni moja: Kumsaidia kila Mtanzania aweze kufanikiwa kupitia kilimo na ufugaji. Tunashirikiana na wadau mbalimbali kama Koudijs Feed Solutions kuwapatia elimu ya lishe bora, mifumo ya ufugaji, na mbinu sahihi za uendeshaji wa miradi ya nguruwe.



Ikiwa nawe unataka kuanzaumeshindwa mara ya kwanza, au unahitaji maarifa zaidiusiache kututafuta.

👉 Bonyeza hapa kuwasiliana nasi moja kwa moja kwa WhatsApp: https://wa.me/255764148221


Usikose nafasi hii. Anza leo! Ufugaji wa nguruwe unaweza kuwa mkombozi wa maisha yako ya kiuchumi.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

write your comment here

write your comment here

Post a Comment (0)

buttons=(Accept !) days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top