WAZIRI
 wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amekamata meli ya uvuvi mali ya 
Kampuni ya Buah Naga 1 ya nchini Malaysia na kuitoza faini ya Dola za 
kimarekani 350,000 sawa na Sh.milioni 770 kwa kosa la kukutwa na mapezi 
ya samaki aina ya papa yenye uzito wa kilo 90 bila miili yake.
Ambapo
 hiyo ni kinyume cha Kanuni ya 66 ya kanuni za Mamlaka ya Uvuvi wa 
Bahari Kuu pamoja na kifungu cha18 (2) cha Sheria ya Mamlaka ya Uvuvi wa
 Bahari Kuu ya mwaka 1998 na marekebisho yake ya mwaka 2007.
Meli
 hiyo ilikamatwa Januari 26 mwaka huu baada ya kufanyika ukaguzi 
uliosimamiwa na kikosi maalum cha kupambana na kudhibiti uvuvi haramu na
 utoroshaji wa samaki na mazao yake wakati ikifanya shughuli za uvuvi 
katika ukanda wa Bahari Kuu kati ya Mkoa wa Lindi na Mtwara.Pamoja na 
kukutwa na mapezi hayo ya papa, meli hiyo ilikutwa pia na bastola aina 
ya Bereta ikiwa na risasi 10 bila ya kuwa na nyaraka za umiliki wake.
Akizungumza
 mjini Mtwara ambako meli hiyo ndiko inakoshikiliwa na Serikali Waziri 
Mpina ameagiza fedha hizo zilipwe ndani ya siku saba huku akitoa onyo 
kali kwa wamiliki wa meli waliopewa leseni za uvuvi wa Bahari kuu 
kufuata masharti ya vibali vyao na katika zama hizi za utawala wa Rais, 
Dk.John Magufuli watachukuliwa hatua kali zaidi.
"Enzi
 za Serikali ya Awamu Tano ya Rais Magufuli mtakaguliwa na kupekuliwa 
kuliko wakati wowote, hivyo ni vizuri mkatii sheria za nchi kwa mujibu 
wa leseni zenu,"amesema Mpina huku akisilizwa na Kapteni wa meli hiyo 
Han Ming Chuan  raia wa Taiwan.
Mpina
 amesema meli hizo zimekuwa zikitumika pia kufadhili biashara nyingine 
haramu ikiwemo kusafirisha dawa za kulevya ,usafirishaji haramu wa  
binadamu na biashara ya silaha.Pia zinatumika kutorosha nyara za 
Serikali ikiwemo meno ya tembo, samaki na madini.
Aidha
 Waziri Mpina amesema kitendo cha wamiliki wa meli hiyo kuwakata samaki 
hao mapezi na kisha kutupa miili yao baharini kimeleta athari kubwa kwa 
Taifa kwani samaki hao wangeweza kutumika kwa matumizi mengine ya 
binadamu na kuchochea uchumi wa nchi.
Hivyo,
 ameridhia faini hiyo iliyotozwa na Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu ya 
Sh.milioni 770 na kuagiza kilo 90 za mapezi ya samaki na samaki 
wasioruhusiwa wataifishwe na kugawiwa kwa wananchi wa maeneo jirani ya 
Manispaa ya Mtwara. "Siku nyingine Serikali ikikamata meli iliyofanya 
makosa ya aina hiyo itataifishwa pamoja na vitu vyote vitakavyokuwemo 
kwa mujibu wa Sheria za nchi,"amesisitiza.
Waziri
 Mpina ameagiza wenye meli hizo kuzingatia masharti ya leseni zao 
zinazotaka kuwepo na asilimia 10 ya mabaharia wa kitanzania ndani ya 
meli zinazoingia kuvua katika Bahari kuu upande wa Tanzania.
Kwa
 upande wa Kamishna wa Oparesheni wa Mamlaka ya kudhibiti na kupambana 
na Dawa za kulevya, Luteni Kanali Fredrick Milanzi amesema meli hiyo 
baada ya kukaguliwa imekutwa na mapezi kilo 90 ya samaki aina ya papa na
 bastola yenye risasi 10 ambayo inaendelea kushikiliwa na Ofisi ya Mkuu 
wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Mtwara hadi hati za umiliki 
zitakapowasilishwa.
Pia
 mwenye meli atatakiwa kuhakikisha anawasafirisha mabaharia kurudi nchi 
zao kwa madai hawataki kuendelea kufanya kazi kutokana na kukiukwa kwa 
mikataba yao ya kazi.Aidha samaki wasioruhusiwa kuvuliwa kwa mujibu wa 
leseni ya uvuvi iliyopewa meli hiyo ( Bychatch) watabaki kuwa ni wa 
Tanzania na watauzwa kwa mnada na fedha zitakazopatikana kiasi cha sh 
milioni 12 zitaingizwa kwenye Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA).
Naye
 Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari Kuu, Hosea Mbilinyi 
amesema hatua zinachukuliwa kwa sasa zimelenga kudhibiti uvuvi haramu na
 utoroshaji wa samaki na mazao yake nje ya nchi na kwamba operesheni 
hizo ni endelevu na hazitambakiza mtu hata mmoja.
Wakati
 huohuo, Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
 Divisheni ya Mashtaka Makao Makuu Dar es Salaam, Wankyo Simon amesema 
makosa hayo adhabu yake ni kubwa na wanapaswa kuzingatia muda uliotolewa
 na Waziri wa kulipa faini.
 Waziri
 wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina pamoja na Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya
 Mtwara Francis Mkuti wakionesha baadhi ya Samaki waliovuliwa na Meli 
hiyo.
 Hosea
 Mbilonyi Kaim Mkurugenz mamlaka ya Usimamiz wa Bahari Kuu  DFSA 
akimuonesha waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina shehena ya Samaki  
tani 4.5 wasiotakiwa kuvuliwa ambao wanatakiwa Kupigwa Mnada Siku 
Yoyote. 
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akilekea katika Meli Buah Naga one kukagua Samaki walivuliwa kinyume na Taratibu.. 





 
 
 
 
 
Great post thankyoou
ReplyDeletewrite your comment here