KILIMO BORA CHA VITUNGUU SAUMU

     UTANGULIZI
Vitunguu saumu ni jamii ya vitunguu maji asili yake ni nchi za Asia lakin pia usitawi katika nchi za kitropik kwa hapa tanzania ustawi katika mikoa ya singida,Arusha,Iringa na Mbeya. pia utumika kama kiungo cha chakula dawa kwa binadamu na wanyama pia na pia utumika kutengeneza mafuta pia harufu yake kali ufukuza wadudu waalibifiu shambani.
hivyo shamba la vitunguu swaumu haliwi na wadudu wa halibifu sana ukiringanisha na mazao mengine.

  AINA YA VITUNGUU SAUMU
Kitaalam bado aijafahamika kunaaina ngapi za vitunguu saumu lakini kuna aina mbili ambazo zinalimwa hapa nchini ni Kienyeji na kisasa.
Aina ya kisasa uzaa vitunguu vikubwa venye ngozi nyeupe napia aina ya kienyeji uzaa vitunguu vyekundu vyenye harufu kali sana na pia havia haribiki mapema ukilinganisha na vya kisasa
vitunguu saumu havizai mbegu halisi kwa hyo uzalishwa kwa kutumia vikonyo vyake
  
     TABIA YA MMEA
Tunguu la vitunguu saumu utokana na vikonyo na hiv vikonyo ndo vinatumika kama mbegu

HALI YA HEWA
Vitunguu saumu ulimwa kiasi cha mita 1800 au zaidi kutoka usawa wa bahari na mvua kiasi cha mm 1000 au zaidi na joto kiasi udongo tifutifu na mnyevunyevu na usio tuamisha maji ndio unafaa kulima vitunguu saumu.
KUANDAA SHAMBA
Andaa shamba mapema lima na akikisha udongo ni tifutifu na pia  unaweza kutuengeneza matuta kwaajili ya kupanda weka samadi shambani wiki 2 kabla ya kupanda au wakati wa kupanda pandia TSP kilo 40 kwa eka au kilo 100 kwa hekta
KUPANDA
 Panda vikonyo vilivo anza kuchipua vilivo safi na visivyo na dalili ya ugonjwa kwa nafasi ya sm 5 kikonyo hadi kikonyo na sm 15 mstari hadi mstari.

PALIZI NA MATUMIZI YA MBOLEA
Palizi ya kwanza ifanyike mapema mara tu magugu yanapo tokeza wakati vikonyo vimesha chipua  na baada ya palizi ya kwanza weka mbolea ya kukuzia CAN au UREA. CAN kiasi cha kilo 75 kwa eka au 190 kwa Hekta au UREA kiasi cha kilo 40 kwa eka na 100 kwa hekta na palilia mara mbili au zaidi ili kuweka shamba katika hali ya usafi
unaweza kupulizia dawa ya kuua magugu endapo vitunguu vimeshaota  kama vile Bromoxynil ambayo uua majani mapana na fusilade uua nyasi.

MAGONJWA
  • fusari muozo-unasababishwa na ukungu katika majani au miziz na pia unaweza kudhibiti kwa kuchoma masalia ya mimea baada ya kuvuna
  • kutu ya majani-mmea unakua na vinundu vya ukngu vyenye rangi ya kahawia kama kutu katika majani tumia dawa ya ukungu  kama fungaran nabayfidan na nordox ili kuzuia
  • kuoza kwa vitunguu-ukungu wa rangi ya blue ufunika vitunguu na usabibisha vitunguu kuoza na utokea gharan vuna kwa uangalifu ili kuepusha michubuko  na hakikisha store ni safi
  • baka jani-vidonda vidogo hutokeza katika majani na badae vinakua vikubwa epuka kumwagilia maji mengi kupita kiasi na tumia mzunguko wa mazao
  • muozo shingo-shingo kuonyesha dalili ya majimaji weka mbolea ya ntrogen kama CAN,UREA na mwagilia maji ya kutosha hasa vinapo elekea kuvunwa
 WADUDU
Wadudu kama chawa wekundu nondo na funza  wanakata miche na mizizi tumia dawa ya karate,selecron,novthin,dursban hutumika kuuwa wadudu

KUVUNA
Vitunguu uvunwa vikifika miezi 6-7 baada ya kupanda majani na mashina unyesha dalii ya kukauka viache vitunguu shambani mpaka majani yanap kauka kabisa  ngoa kwa mkono au jembe na pia kua muangalifu ili kuepusha kuchubua vitunguu
 







 



16 comments

Unknown said...

asante kwa elimu

Unknown said...

Maeneo ya moshi kitunguu swaumu kinakubali?

Rubaba Imani said...

ndio kwa moshi vnakubali pia

katewapps said...

morogoro naweza lima?

vcvcvcvcv said...
This comment has been removed by a blog administrator.
Rubaba Imani said...

asante ndugu emmanuel
nnacho taka kukuelekeza ni kwamba
kuvunwa kwa mazao inategemea na eneo husika pamoja na aina ya mbegu,
mfano mdogo mahind ya mda mrefu uchukua miez 6 kuvunwa ila kwa mikoa mingine kama mbeya huchukua had miez 8

FRANCIS KITANGE said...

Je kwa maenei ya meru kitunguu swaumu kinaweza kustawi

Rubaba Imani said...

bila shaka ndugu francis proches

Makungano said...

Asante sana kwa very brief but rich meseji

Unknown said...

Asante kw meseji Nzuri Mbegu zinapatikana wap hasa kwa Arusha??

Anonymous said...

Naomba Kuuliza nimevutiwa sana na maada hii je kwa mkoa wa Mara hili zao linaweza kustawi pia?

MICAHEL said...

Naomba Kuuliza nimevutiwa sana na maada hii je kwa mkoa wa Mara hili zao linaweza kustawi pia?

IMANI LUBABA said...

ndugu MICAHEL ni vyema kuwasiliana na wataalamu wa udongo ili kufahamu mazao yanayo sitawi vizuri katika mkoa wako.

DEOGRATIAS EMMANUEL, ili kufahamu mahali mbegu zinapopatikana unaweza kutembelea agrovet katka mkoa wako.

MAKUNGANO, asante kwa kua nasi

Unknown said...

Je?kwatanga inawezekana

Giant said...

Asante sana kwa maarifa haya ya msingi

Unknown said...

nimesoma na.kuelewa maelezo yako ..je dar es salaam inafaa kupanda zao hili