WAKULIMA WA MAHARAGE WANAWEZA KUPUNGUZA UPOTEVU WA MAHARAGE KWA KUBADILI MBINU ZA UVUNAJI NA USAFIRISHAJI


Ni msimu wa mavuno kanda ya kaskazini magharibi mwa Tanzania. Monica Lugesha akiwa amvaa vazi buluu ya kung’aa na waridi na kitambaa. Mama huyu wa miaka 70 anaonekana akiwa akivuna maharage, anafurahia matunda ya kazi yake. 

Bi. Lugesha anaishi wiliya ya Ngara kata ya Rulenge. Anasema, wakulima wengi wanapoteza maharage yao wakati wanapovuna shambani na wanaposafirisha maharage.

Bi. Lugesha anajaribu kupunguza upotevu wa maharage wakati wa kuvuna na kusafirisha. Anasema, “Nina vuna maharage yangu na kuyasafirisha nyumbani kwangu. Hapo nyumbani nina anika maharage yangu katika turubai.” 

Anasema wakulima wengi wanavuna maharage kwa kung’oa shina zima na kufunga mashina hayo kwa kamba na nisha kusafirisha kwa kubeba kichwani kupeleka nyumbani. Anaelezea: “Chochote tunachokivuna tunakipoteza kwasababu vibebea vya maharage vinapasuka na mbegu kudondoka shambani. Wakulima wengine wanasafirisha maharage kwa kutumia pikipiki au baisikeli, na maharage mengi yanadondoka njiani.” 

Mastidia Venus pia ni mkulima wa maharage wilayani Ngara. Mkulima huyu wa miaka 40 anasema wakulima wanaweza kupoteza mpaka kilo 10 za maharage katika shamba la hekari moja wakati wa kuvuna na kusafirisha. 

Adronizi Bulindoli ni mkulima mwingine wa maharage wilayani Ngara. Anasema wakulima wengi wilayanai wanavuna maharage shambani wakti yakiwa yamekauka sana, ambapo inasababisha vibebea/vifuko vya maharage kupasuka na kudondosha mbegu shambani.

Bw. Bulindoli anasema ni vigumu sana kuokota mbegu za maharage shambani zinapodondoka, anawashauri wakulima wengine wavune maharage wakati wa asubuhi amabapo jua sio kali sana.
Essau Nyamziga ni afisa ugani wa eneo hili. Anakubaliana na Bw. Bulindoli kwamba kuvuna maharage pindi yanapokuwa yamekauka sana inapelekea kupoteza mbegu za maharage na hivyo kupata hasara. Anawahimiza wakulima kuvuna maharage pindi yanapobadili rangi na kuwa ya kijivu na kutumia mifuka kusafirisha na kuhifadhi maharage. 

Constatine Mdende ni afisa kilimo umwagiliaji wa wiliya ya Ngara. Anakadiri kuwa kiasi cha tani 46,000 za maharage zitavunwa mwaka huu katika wilaya yake, na kati ya tani hizi, tani 2,300 zitapotea. Anasema wakulima wabebe maharage katika mifuka imara ya plastiki kuepuka kudondoka kwa mbegu za maharage wakati wa kuvuna na kusafirisha. 

Mbali na kumtegemea maafisa ugani kutoka wiliayani kuwapatia elimu, wakulima wanapaswa kupata elimu kutoka vyanzo mbadala kama vipindi vya kilimo redioni. Frank Ademba ni afisa miradi wa shirika la Farm Radio International, sjirika lisilo la kiserikali linalofanya kazi hapa wiliyani na Redio Kwizera kuzalisha vipindi vya kilimo redioni. Anasema vipindi vya redio vinawashawishi wakulima kulima maharage, ikigusia mada za upandaji, mavuno, kupunguza upotevu wa mazao baada ya mavuno na masoko. 

Mkulima mmoja wapo aliye weza kusikiliza vipindi na kubadili namna ya uzalishaji, uvunaji na uhifadhi wa maharage ni Sophia Metusera kutoka kijiji cha Kumuzuza wilaya ya Ngara. Akiwa anatembea katika shamba lake akibeba mbegu zilizo vunwa za maharage katika mifuko yeye na wenzake, anasema, “Nina pendelea kusafirisha mbegu za maharage kuliko kusafirisha [mmea mzima wa maharage], kwasababu kubeba mmea mzima wa maharage vibebea vinaweza kupasuka na kudondosha mbegu za maharage.”
Bi. Metusera anasema anasema alijifunza namna ya kuzalisha maharage kupitia vipindi vya Redio Kwizera. Anaongeza, “Nataka kuwa mkulima bora kijijini kwangu.”

No comments