WAFUGAJI WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUWAKUMBUKA UJENZI MADARASA

 Wafugaji jamii  ya Kimasai Kitongoji cha Manyara kijiji cha Twatwatwa  wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro wamempongeza Rais Samia kwa kuwakumbuka jamii hiyo ambayo ilisahaulika katika sekta ya elimu kwa kuwajengea madarasa matatu kupitia  mradi wa Covid 19


Akizungumza katika hafla hiyo Chifu mkuu wa  mikoa saba wa Kabila hilo la Wamasai  Chifu Kashu Moreto amesema wanamshukuru Rais Samia kwa  na kuahidi kumuunga mkono

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kilosa Alhj Majd Mwanga amewataka wazazi kuacha tabia ya kuwaozesha watoto wa kike  huku Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi akiahidi kushirikiana na jamii hiyo katika kuinua elimu kwa jamii hiyo ya kifugaji.


No comments